Monday, 22 May 2017

Marufuku ya uuzaji wa nyama ya mbwa yasababisha wasiwasi China

Marufuku ya uuzaji wa nyama ya mbwa yazuia wasiwasi katika hafla ya Yulin China
Sherehe ya kula nyama ya mbwa nchini China ilio na umaarufu kwa ukatili wa wanyama mwaka huu itapigwa marufuku kuuza nyama ya mbwa.
Ulaji wa mbwa nchini China sio haramu na wauzaji wa nyama hiyo tayari wameanza kulalamikia marufuku hiyo wengine wakisema hawajaisikia .
Sherehe hiyo inayofanyika mwezi Juni kila mwaka imekuwa ikivutia pingamizi kubwa kutoka kwa wanaharaki wa wanyama wanaosema kuwa wanyama hao hufanyiwa ukatili.
Inakadiriwa kuwa katika sherehe hiyo ya Yulin iliofanyika miaka michache iliopita, takriban mbwa na paka 10,000 walichinjwa na kufanywa kitoweo wakati wa sherehe hiyo ya siku kumi.
Lakini idadi hiyo imekuwa ikipungua katika siku za hivi karibuni huku pingamizi ikiendelea nchini China na kimataifa.
Wanaharakati kadhaa wa wanyama wanasema kuwa wauzaji na mikahawa wameambiwa kwamba hakuna nyama ya mbwa itakayouzwa wakati na kabla ya sherehe hiyo.
Peter Li, mtaalamu wa sera za China aliambia BBC kwamba mamlaka tayari imejaribu kuwakatisha tamaa wanaotekeleza hatua hiyo ,na kwamba mwaka huu itawapiga faini watakaokiuka marufuku hiyo.
Raia wa China wakila nyama ya mbwa wakati wa sherehe ya Ylin nchini humoHaki miliki ya pichaAFP
Image captionRaia wa China wakila nyama ya mbwa wakati wa sherehe ya Ylin nchini humo
Sheria hiyo itaathiri wauzaji wa nyama ya mbwa, wafanyibiashara na wenye mikahawa.
Lakini marufuku hiyo itakuwa ya muda ikimaanisha kwamba mbwa wengi wanaweza kuchinjwa kabala ya sherehe hiyo.
''Bado kuna pingamizi kutoka kwa wafanyibiashara wa nyama hiyo ya mbwa'', alisema bwana Li.
''Kote nchini walikuza ulaji wa nyama ya mbwa kama utamaduni wa kitaifa pamoja na chakula cha Wachina.
Hilo sio la kweli ,baraza la mji wa Yulin haliweza kufanya kitu kama hicho kwa kuwa kitasababisha wasiwasi mkubwa kwa kijamii.
source:bbc

Related Posts:

  • Bomba la kupitisha pombe kujengwa UjerumaniHaki miliki ya pichaAFPImage captionPombe itakuwepo kwa wingi katika tamasha hilo Waandalizi wa Tamasha maarufu la muziki wa rock nchini Ujerumani wamewahakikishia wateja zaidi ya elfu 75 kwamba, katu! hawatokumbwa na kiu ya … Read More
  • Gavana asema al-Shabab huenda wakateka eneo la KenyaImage captionRamani ya Somalia Viongozi wa eneo la mashariki nchini Kenya wameonya kwamba maeneo ya taifa hilo huenda yakanyakuliwa na wapiganaji wa Al-Shabab. Gavana wa kaunti ya Wajir ambayo inapakana na taifa la Somalia a… Read More
  • Marekani kufanya majaribio ya kudungua komboraImage captionMfumo wa kudungua makombora wa Marekani uliopelekwa Korea Kusini Idara ya jeshi nchini Marekani kwa mara ya kwanza itajaribu kudungua kombora la masafa marefu lililo na uwezo wa kufyatuliwa kutoka bara moja hadi … Read More
  • Dwayne 'The Rock' Johnson kuwania urais Marekani mwaka 2020?Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionMwigizaji na mwanamiereka Dwayne 'The Rock' Johnson Dwayne 'The Rock' Johnson kuwania urais mwaka 2020? Dwayne 'The Rock' Johnson alitangaza kuwa atawania urais wa Marekani mwaka … Read More
  • Trump 'atengwa' na wenzake G7Image captionRais Trump ametengwa na wenzake kuhusiana na makubaliano ya tabia nchi yaliofakiwa mjini Paris Viongozi katika mkutano wa G7 wametofautiana kuhusu taarifa ya mabadiliko ya tabia nchi. Viongozi sita walikubaliana… Read More

0 comments:

Post a Comment