Thursday, 25 May 2017

Mbunifu wa Nembo ya Taifa ahamishiwa Hosptali ya Muhimbili


Mzee Francis Ngosha ndiye mchoraji na mbunifu wa nembo ya taifa maarufu kama Bibi na Bwana, S iku mbili zilizopita aliliripotiwa kuwa anaishi maisha ya Magumu huko Buguruni jijini Dar es salaam. Kibanda alichokuwa akiishi ni cha hovyo sana mithili ya  banda la kuku limezungushwa na Bati juu mpaka chini.

Baada ya taarifa hiyo kutolewa na vyombo vya habari, Serikali imesema kuanzia sasa itaanza kumpatia huduma za matibabu na kijamii Mzee Francis Ngosha, mbunifu wa Nembo ya Taifa ya bibi na Bwana.

Ambapo Mzee Ngosha amehamishiwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) akitokea Amana alikokuwa amelazwa tangu jana (Jumatano).

Ngosha amehamishwa hospitalini hapo baada ya Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Hamisi Kigwangalla kumtembelea leo asubuhi kumjulia hali.

Katika mazungumzo, Ngosha amesema alichora nembo hiyo akiwa na mwenzake Ali Pangani ambaye amefariki dunia.

"Nimetumwa nije kumuona mzee wetu aliyechora nembo ambayo ni utambulisho wa Mtanzania, tumemuhamisha hapa na kumpeleka Muhimbili kwa matibabu zaidi," anasema Dk Kigwangalla.
source:muungwana

Related Posts:

  • Al Shabab wavamia mji wa Mandera Kenya Kundi la wanamgambo wa al-Shabab limevamia eneo la Omar Jillo lililoko mji wa Mandera unaopakana na Somalia usiku wa kuamkia leo. Al-Shabab limemuua afisa huyo, Chifu ws eneo Dekow Adan na kuwateka maafisa wawili wa kiteng… Read More
  • Sababu ya Chui kula windo lake akiwa juu ya mti? Chui akimuwinda Swara Wanyama wengi wakiwemo wanyama wakubwa watano wa Afrika, hurandaranda katika mbuga ya wanyama pori ya Sabi Sand nchini Afrika Kusini. Wakati mwingine wanyama hawa hupatikana maeneo wasiyotarajiwa, kam… Read More
  • Uwezekano wa mimea ya msituni kutumiwa kupanga uzazi Je huenda kemikali kutoka kwa mimea ya msituni ikawa dawa mpya ya kupanga uzazi Kemikali mbili zinazopatikana katika mimea ya mistuni zinauwezo wa kutengeneza dawa za mpango wa uzazi, ikiwa wanasayansi wangejua wapi wangepa… Read More
  • Serikali ya Kenya yapunguza bei ya unga wa mahindi Imekuwa ni afueni kwa Wakenya baada ya serikali kutangaza kupunguzwa kwa bei ya unga na kuondoa ushuru unaotozwa kwa bidhaa kama vile maziwa na sukari. Kwenye kikao na waandishi mjini Nairobi, Waziri wa kilimo nchini humo,… Read More
  • Majaji wawili wa Mahakama Kuu waacha kazi Tanzania Rais Magufuli ameridhia maombi ya watatu hao kutaka kuacha kazi Majaji wawili wa Mahakama Kuu nchini Tanzania wameacha kazi, kwa mujibu wa taarifa kutoka ikulu. Taarifa hiyo inasema majaji Aloysius Kibuuka Mujulizi na Upen… Read More

0 comments:

Post a Comment