Thursday, 25 May 2017

Ujumbe wa Diamond Baada ya Ivan kufariki Dunia

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Diamond Platnumz ameandika ujumbe huu "Mbele yako, Nyuma yetu" Ujumbe huo ni baada ya Aliyekuwa mume wa Zarina Hassan ‘Zari The Bosslady’, Ivan Semwanga kufariki dunia akiwa hospitali nchini Uganda alipokuwa amelazwa kutokana na matatizo ya moyo usiku wa kuamkia leo Mei 25, 2017.

Ivan aliyekuwa baba wa watoto watatu wa kiume wa Zari, aliachana na mwanamama huyo miaka michache iliyopita ambapo Zari alihamishia mapenzi kwa mwanamuziki Diamond Platinumz ambaye mpaka sasa wamezaa  watoto wawili, wa kike mmoja na wa kiume mmoja.

Ivan alikuwa maarufu Afrika Mashariki kutokana na biashara zake kubwa alizokuwa akifanya zikiwemo umiliki wa vyuo mbali mbali nchini Afrika Kusini, pamoja na Tycoon Ivan.

Related Posts:

  • Kashfa nzito zaikumba Wizara ya maliasili BAADHI ya wabunge wamelalamikia vitendo vinavyofanywa na Wizara ya Maliasili na Utalii, kukamata na kupiga mnada mifugo inayoingia kwenye hifadhi za taifa. Kutokana na vitendo hivyo, watunga sheria hao wameishauri serik… Read More
  • Msanii aliyebuni nembo ya Taifa sakata lake latua bungeni Dodoma. Bunge jana lilielezwa kuwa msanii aliyebuni na kutengeneza nembo ya taifa ya Bibi na Bwana, Francis Ngosha ametelekezwa na taifa na anaishi maisha magumu.Suala la msanii huyo liliibuka Bungeni mjini Dodoma leo, kuto… Read More
  • Mauaji Pwani yamepangwa: Mbunge Dodoma. Mauaji katika wilaya za Kibiti na Rufiji jana yaliibuka bungeni kwa mara ya pili, wakati mbunge wa Rufiji (CCM), Mohamed Mchengerwa alipoeleza siri ya mipango na kiini chake.“Nataka niseme na Rais wangu ajue. Mambo … Read More
  • Wajumbe wa kamati Iliyomng'oa Muhongo walitishwa RAIS Dk. John Magufuli amebainisha kuwa licha ya kamati ya Kuchunguza Makontena ya Mchanga wenye Madini (makinikia) kupewa ulinzi mkali, kulikuwapo vitisho na hata baadhi ya wajumbe kutaka kuhongwa. Akizungumza jana wak… Read More
  • Kikwete aanza kazi na Mgogoro wa Libya Rais Mstaafu Jakaya Mrisho kikwete ameanza kazi kama Mwenyekiti Mwenza katika Baraza la Kimatifa la Wakimbizi ambapo ameanza kazi yeye na jopo lake ya kutaka kusuluhisha Mgororo wa muda mrefu wa nchin ya Libya. Kikwete … Read More

0 comments:

Post a Comment