Msanii wa Nikki wa Pili, amempongeza Rais Magufuli kwa kitendo alichokifanya leo cha kumtumbua Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Mwijarubi Muhongo na kumwambia Mungu amsimamie katika kupambana na ufisadi.
Niki ametoa salamu hizo za pongezi kupitia ukurasa wake wa kijamii instagram kwa kusema watanzania wanaopewa dhamana wasipoamua kuwa waadilifu umaskini utaweza kuandika historia tukufu kwa Tanzania.
"Wizi mkubwa utamkuta mwekezaji na wakala wake wa kitanzania (wasomi, viongozi, wafanya biashara) yaani ni kama ule uchumi wa kikoloni manufaa ni kwa kampuni ya nje na kitabaka cha watanzania wachache...Nimpongeze Mkuu wa nchi kwa kuamua kupambana na ufisadi huu...Ila vita ya kuvunja mfumo wa kiuchumi wa kifisadi ni hatari...Kina Lumumba, Sankara huko Chile, Nikaragwa, Venezuela, Haiti, Iran...Viongozi hawakupona ni vita kuu Mungu akusimamie". Ameandika Nikki wa Pili.
Wednesday, 24 May 2017
Home »
» Nikki wa Pili ampongeza Rais Magufuli
Nikki wa Pili ampongeza Rais Magufuli
Related Posts:
MEYA, WAMILIKI WA SHULE NA WAANDISHI WAKAMATWA WAKIWA SHULE YA LUCKY VINCENT Meya wa Jiji la Arusha, Kalist Lazaro, wamiliki wa shule binafsi pamoja na waandishi wa habari na wadau wengine wamekamatwa na Polisi wakati wakikabidhi rambirambi na kutoa pole leo kwenye shule ya Lucky Vincent. Kwa muji… Read More
Rwanda yaitoza MTN faini ya dola milioni 8 Kampuni kubwa ya mawasiliano ya MTN tawi la Rwanda imetozwa faini ya zaidi ya dolla milioni 8 za Marekani kwa kile kilichotajwa kuwa kukiuka makubaliano baina yake na serikali ya nchi hiyo. Kampuni hiyo yenye wateja takrib… Read More
Trump aipa Tanzania $526m kukabiliana na ukimwi Serikali ya Marekani kupitia ofisi ya rais Donald Trump imetangaza kupatia Tanzania ufadhili wa kukabilana na virisu vya ukimwi. Marekani, ambayo siku chache zilizopita ilitangaza kusimamisha ufadhili wake kwa wizara ya af… Read More
TISA MBARONI KWA KUVUNJA NYUMBA, WIZ JESHI la Polisi Mkoa wa Mwanza linawashikilia watu tisa kwa tuhuma za kujihusisha na uvunjaji wa nyumba na kuiba mali wilayani Ilemela. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed… Read More
SIRI YA MAJAJI KUACHA KAZI NI HII HATUA ya majaji wawili wa Mahakama Kuu ya Tanzania kuacha kazi kwa wakati mmoja imezua mjadala. Moja ya jambo kubwa lililojitokeza kuhusu hatua hiyo, ni tuhuma za kuhusishwa na kashfa ya Akaunti ya Tegeta Escrow, huku mwi… Read More
0 comments:
Post a Comment