Wednesday, 24 May 2017

Trump asababisha Al Jazeera kufungiwa Saudi Arabia

Saudi Arabia imeifungia mitandao ya Al Jazeera na Magazeti ya Qatar baada ya Rais wa Qatar Tamim Bin Hamad Al-Thani kusema anaishangaa Saudi Arabia kumkaribisha Rais wa Marekani Donald Trump kauli iliyopingwa na Mfalme wa Saudi Arabia.

Sehemu ya taarifa ya Rais wa Qatar kupinga ziara ya Trump Saudi Arabia ilisomeka: >>>“Rais Trump hawezi kukaribishwa Qatar na ninaishangaa Saudi Arabia kumkaribisha mtu kama Trump ambaye anashtakiwa kwa makosa ya kihalifu nchini kwake. Mimi naitambua Serikali ya Iran kama Serikali ya Kiislamu kama Marekani haiitambu si lazima kukubaliana nao.”

Mtandao wa Al Jazeera umefungiwa kwa sababu unamilikiwa na Serikali ya Qatar jambo ambalo limewafanya watumiaji wa mtandao huo Saudi Arabia kupata shida ambapo kila wakijaribu kuingia kwenye mitandao hiyo wamekuwa wakikutana na ujumbe uliowatahadharisha kuwa mitandao hiyo imefungiwa.

Related Posts:

  • Obama anunua nyumba ya $8.1m ya kuishi Washington DCHaki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionMali ya Obama ikihamishiwa Washinton baada yake kuondoka White House mwezi Januari Familia ya Rais mstaafu wa Marekani Barack Obama imenunua nyumba ambayo kwa muda wamekuwa wakiish… Read More
  • Viongozi wa Afrika wamlaumu Trump kuupuza mkataba wa ParisImage captionRais wa zamani wa Ghana John Mahama (pichani) alikuwa ni miongoni mwa viongozi wa dunia waliounga mkono makubaliano hayo ya kihistoria juu ya mazingira mjini Paris 2015 Rais wa zamani wa Ghana John Mahama amelaan… Read More
  • Wanajeshi wakichoma moto kituo cha polisi NigeriaHaki miliki ya pichaNIGERIAN POLICEImage captionKituo cha polisi kilichochomwa moto Nigeria Ripoti kutoka nchini Nigeria zinasema Maafisa wa jeshi la Wanamaji wamevamia na kuchoma moto kituo cha polisi mjini Calabar kusini mw… Read More
  • Jeshi la Polisi Tanzania, latoa onyoImage captionMkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania Simon Sirro Jeshi la Polisi nchini Tanzania limetoa onyo kwa wale wote wanaojihusisha na vitendo vya uhalifu na kusababisha mauaji ya raia na polisi. Akizungumza kwa mara ya kwan… Read More
  • Reli mpya ya kisasa SGR yazinduliwa KenyaImage captionReli mpya ya SGR yazinduliwa Kenya Kenya imezindua reli mpya kati ya mji wa Mombasa hadi Nairobi ikiwa ni miezi 18 mapema. Reli hiyo iliotengezwa kupitia ufadhili wa shilingi bilioni 3.2 kutoka serikali ya China… Read More

0 comments:

Post a Comment