Tuesday, 16 May 2017

Sababu ya Chui kula windo lake akiwa juu ya mti?

Chui akimuwinda Swara
Chui akimuwinda Swara
Wanyama wengi wakiwemo wanyama wakubwa watano wa Afrika, hurandaranda katika mbuga ya wanyama pori ya Sabi Sand nchini Afrika Kusini.
Wakati mwingine wanyama hawa hupatikana maeneo wasiyotarajiwa, kama twiga mdogo ambaye waelekezi walimpata juu ya mti akiwa amekufa.
Chui mkubwa alimuua twiga huyo kisha akampandisha mita kadha juu ya mti. Alisherehekea chakula hicho kwa siku chache na kuacha tu mifupa, ngozi na nyama nyama zikiwa zimetapakaa.
Twiga huyo alikuwa na uzito wa kila 300 karibu na uzito mara tano zaidi ya Chui.
Ikiwa Chui hatompandisha mnyama huyo mtini basi ako kwenye hatari ya kumpoteza kwa fisi na simba.
Ikiwa Chui hatompandisha mnyama huyo mtini basi ako kwenye hatari ya kumpoteza kwa fisi na simba.
Ni kitu ambacho kinaeleweka kuwa kisicho cha kawaida kufanyika lakini Chui ana sababu nzuri ya kuweza kufanya hivyo.
Ikiwa Chui hatompandisha mnyama huyo mtini basi ako kwenye hatari ya kumpoteza kwa fisi na simba.
Kumpandisha juu ya mtu humsadia Chui kuzuia chakula chake kuibiwa kwa mujibu wa utafiti uliofanywa mwezi Februari mwaka 2017.
Utafiti uliofanywa na shirika moja lisilokuwa la serikali uligundua kuwa chui katika mbuga ya Sabi Sands huwawinda karibu familia 40 ya wanyama
Chui hupandisha mtini nusu ya wanyama anaowawinda. Pia hupoteza moja ya mawindo yake kati ya matano kwa wanyama wengine kama fisi, simba na hata chui wa kiume.
Ikiwa chui ataamua kupandisha mtini windo lake na kisha kugundua hakuna mshindani karibu anawez kumburura kutafuta mti unaofaa ulio karibu
Mara chuo anapokaribia mti hupanda hadi umbali wa mita10 juu kutafuta eneo lililo salama kuning'inisha windo lake.
Hata hivyo wakati mwingine hali huwa ni ya dharura. Kama fisi yuko karibu Chui mara moja anaweza kupanda mti wowote ulio karibu kuzuia chakula chake kuibwa.


source:bbc

Related Posts:

  • Trump 'atengwa' na wenzake G7Image captionRais Trump ametengwa na wenzake kuhusiana na makubaliano ya tabia nchi yaliofakiwa mjini Paris Viongozi katika mkutano wa G7 wametofautiana kuhusu taarifa ya mabadiliko ya tabia nchi. Viongozi sita walikubaliana… Read More
  • Marekani kufanya majaribio ya kudungua komboraImage captionMfumo wa kudungua makombora wa Marekani uliopelekwa Korea Kusini Idara ya jeshi nchini Marekani kwa mara ya kwanza itajaribu kudungua kombora la masafa marefu lililo na uwezo wa kufyatuliwa kutoka bara moja hadi … Read More
  • Gavana asema al-Shabab huenda wakateka eneo la KenyaImage captionRamani ya Somalia Viongozi wa eneo la mashariki nchini Kenya wameonya kwamba maeneo ya taifa hilo huenda yakanyakuliwa na wapiganaji wa Al-Shabab. Gavana wa kaunti ya Wajir ambayo inapakana na taifa la Somalia a… Read More
  • Taarifa ya leo Mei 28, kumuhusu Ivan aliyekuwa Mume wa Zari IVAN SEMWANGA, aliyekuwa mume wa Zarina Hassan ‘The Bosslady’ ambaye sasa ni mpenzi na mzazi mwenzake wa mwanamuziki wa Tanzania, Naseeb Abdul ‘Diamond Platnum’, atazikwa Jumanne (Mei 30) wiki ijayo  nyumbani kwao Kay… Read More
  • Wauawa kwa kuwalinda wanawake Waislamu MarekaniHaki miliki ya pichaCBS/EVNImage captionPolisi wanasema mwanamume aliyekuwa akitukana, aliwageukia wanaume hao waliojaribu kuingilia kati Polisi katika mji wa Portland nchini Marekani, wanasema wanaume wawili waliuawa, walipo… Read More

0 comments:

Post a Comment