Thursday, 18 May 2017

MAPENZI YANA NGUVU:Mwanamfalme aacha ufalme ili kuolewa na mtu wa kawaida

Binti wa mfalme nchini Japan, Mako, ameamua kuacha maisha ya kifalme kwa ajili ya mapenzi.
Binti wa mfalme nchini Japan, Mako, ameamua kuacha maisha ya kifalme kwa ajili ya mapenzi.
Binti wa mfalme nchini Japan, Mako, ameamua kuacha maisha ya kifalme kwa ajili ya mapenzi.
Hii ni baada ya mwanamfalme Mako, ambaye ni mjukuu wa mfalme Akihito, kukubali kuoana na Kei Komuro ambaye ni mwananchi wa kawaida nchini mwao.
Wawili hao walipendeana baada ya kukutana katika hoteli moja mnamo mwaka wa 2012.
Mwanamfalme Mako mwenye umri wa miaka 25, atafunga ndoa na mfanyikazi wa kampuni ya mawakili, Kei Komuro waliosoma pamoja katika chuo cha Christian University mjini Tokyo.
Sheria za kifalme nchini Japan zinamhitaji yeyote atakayeoana na mtu asiyetoka kwenye kasri, aache ufalme.
Ufalme wa Japan umethibitisha kuwa mipango ya harusi inaendelea lakini itatangazwa rasmi baada ya tarehe rasmi kujulikana.
Hata hivyo, Bw Komuro amedinda kuzungumzia mipango ya harusi. ''sio wakati mwakafaka wa kuzungumza, nitasema muda ufaao,'' alisema.
Hatua hiyo imezua gumzo nchini Japan kuhusu urithi wa ufalme huku mfalme Akihito akikaribia kustaafu.
Hii sio mara ya kwanza hilo kutokea, kwani shangaziye Princess Mako, ambaye pia ni binti pekee wa mfalme akihito, Princess Sayako, alilazimika kuondoka kasrini baada ya kuoana na mpenzi wake mwaka wa 2005.
Alilazimika kujifunza maisha ya kawaida, ikiwemo kuendesha gari na kufanya ununuzi wa bidhaa za nyumba.
Mnamo mwezi Agosti mwaka uliopita, Mfalme Akihito mwenye umri wa miaka 83, alidokeza kustaafu kwake kutokana na umri wake.

source:bbc

Related Posts:

  • Mzee Akilimali ataka kumpiku Manji, atangaza kuwania uenyekiti Yanga AKILIMALI Katibu Mkuu wa Baraza la Wazee wa Yanga, Ibrahimu Akilimali ametangaza kuwania nafasi ya uenyekiti wa klabu ya hiyo iliyoachwa wazi hivi karibuni na aliyekuwa mwenyekiti wa klabu hiyo, Yusuf Manji.Hivi karibuni M… Read More
  • Hili ndilo janga la tatu alilolipata Mbowe Masaibu yanazidi kumkumba Mbunge wa Hai na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe baada ya Serikali kung’oa miundombinu ya umwagiliaji katika shamba lake.Hilo ni janga jingine kwa Mbowe baada ya miezi michache iliyopita kutaj… Read More
  • AJALI:Gari la polisi laua bodaboda Gari la Polisi MTU mmoja amefariki dunia na mwingine kujeruhiwa baada ya pikipiki maarufu kwa jina la bodaboda waliyokuwa wakitumia kusafiri, kugongana uso kwa uso na gari la Jeshi la Polisi katika wilaya ya Rorya… Read More
  • HALI TETE:Chenge agoma kuzungumza Vigogo waliotajwa katika ripoti ya pili ya kuchunguza makontena yenye mchanga wa madini (makinikia)  kuisababishia Serikali hasara ya matrilioni ya fedha kupitia sekta ya madini, walipokuwa wakihudumu katika nyadhifa … Read More
  • SOMA: Ronaldo alivyojitetea kuhusu tuhuma za ukwepaji kodi Mchezaji huyo, jana Jumanne aliandikiwa barua na akitakiwa kujibu mashtaka yaliyoandaliwa na mamlaka ya kodi mjini Pozuelo de Alorcon.Mwanasheria wa Cristiano Ronaldo amepinga vikali tuhuma zinazoelekezwa kwa mshambuliaji h… Read More

0 comments:

Post a Comment