Thursday 18 May 2017

BREAKING NEWS:Watu 18 wafariki kutokana na Ebola DRC

Watu 18 wafariki kutokana na Ebola DRC
Watu 18 wafariki kutokana na Ebola DRC
Jumla ya visa 18 vya ugonjwa wa Ebola vimeripotiwa nchini Jamhuri ya Demokrasi ya Congo kwa mujibu wa shirika la afya Duniani WHO.
Vifo vya watu watatu vimeripotiwa kutokana na ugonjwa huo.
Waliokufa ni pamoja na mwanamume wa umri wa miaka 39 aliyetajwa kuwa "mgonjwa sufuri" na watu wawili ambao walikuwa wamekaribiana naye, WHO ilisema.
WHO iliongeza kuwa takwimu zake zinaonyesha kuwa kuna hatari kubwa eneo hilo na ndogo katika maeneo ya kimataifa
WHO ilitangaza mlipuko wa ugonjwa huo nchini DRC wiki iliyopita.
Zaidi ya watu 11,000 walifariki kutokana na ugonjwa wa Ebola magharibi mwa Afrika mwaka 2014 na 2015 hasa nchini Guinea, Sierra Leone na Liberia.

SOURCE:BBC

0 comments:

Post a Comment