Saturday, 13 May 2017

Shambulizi la uhalifu wa mtandao laathiri mataifa 99 duniani

Hivi ndivyo ilivyokuwa katika baadhi ya kompyuta wakati wahalifu wa mtandao walipotekeleza shambulio
Sambulizi la kihalifu mitandaoni lililotendeka kupitia utumizi wa vifaa vinavyoaminika kuibwa kutoka kitengo cha ujasusi nchini Marekani NSA limeathiri mashirika tofauti duniani.
Kampuni ya kulinda uhalifu wa mitandao Avast, imesema kuwa imeona kesi 75,000 za programu zinazotumika kufanya uhalifu mtandaoni inayojulikana kama 'WannaCry' duniani.
Kuna ripoti za maambukizi katika mataifa 99 ikiwemo Urusi nchini China.
Kati ya mashirika yalioathirika zaidi ni shirika la huduma za afya nchini Uingereza na Uskochi.
BBC inaelewa kwamba takriban mashirika 40 na huduma kadhaa za matibabu ziliathirika huku operesheni na mikutano ikifutiliwa mbali.
Programu hiyo ilisambaa kwa kasi siku ya Ijumaa ambapo ilitaka malipo ya dola 300 ili kufungua faili ilizokuwa imeziteka nyara katika kompyuta.
Siku nzima, mataifa ya Ulaya yaliripoti maambukizi hayo.
Idadi kubwa ya kampuni kubwa ikiwemo Telefonica ,kampuni ya umeme ya Iberdrola na ile ya Gesi asilia pia ziliathirika huku kukiwa na ripoti kwamba wafanyikazi katika kampuni hizo waliagizwa kuzima kompyuta zao.
Raia walipiga picha za kompyuta zilizoathirika katika mtandao wa Twitter ikiwemo mashine ya kukata tiketi za safari ya reli nchini Ujerumani pamoja na maabara ya kompyuta nchini Italy.

source:bbc

Related Posts:

  • Hoja 6 moto mkali kwa serikali bungeni MJADALA wa mapendekezo ya makadirio ya bajeti ya serikali kwa mwaka wa fedha wa 2017/2018 unatarajiwa kuhitimishwa leo mjini hapa huku hoja sita zikionekana kuwa mtihani mgumu kwa serikali kuzitolea majibu kesho wakati in… Read More
  • Simba yatumia Mil. 100/ kumshawishi Niyonzima NI UMAFIA TU! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya kiungo wa Yanga, Haruna Niyonzima kudaiwa kujiunga na Klabu ya Simba kwa mkataba wa miaka miwili baada ya kupewa ofa ya Sh. milioni 100. Habari zilizopatikana jana jioni … Read More
  • Ally Mayay, Mtemi kuwania urais TFF  MAYAY Ally Mayay anatarajia kuchukua nafasi ya kuwania Urais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).Taarifa zinaeleza Mayay ambaye ni mchezaji wa zamani wa Yanga na Taifa Stars, atachukua fomu hizo leo. MTEMI Wa… Read More
  • Zitto aukataa Urais TFF Ijumaa ya Aprili 21, mwaka huu, gazeti la michezo na burudani nchini, Mwanaspoti, liliandika habari kwenye ukurasa wake wa kwanza yenye kichwa: "Zitto ajitosa Urais TFF, Rage amkubali." Upande wangu, licha ya kwamba hab… Read More
  • Nchemba amtolea uvivu Tundu Lissu  Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba ‘amemvaa’ Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu kwamba amejaribu kutengeneza kila aina ya kichaka kukwamisha jitihada za Rais John Magufuli kupambana na usafirish… Read More

0 comments:

Post a Comment