Monday, 15 May 2017

Trump atakiwa kusalimisha kanda za mazungumzo na James Comey

Donald Trump ametakiwa kusalimisha kanda za mazungumzo yaliorekodiwa kati yake na aliyekuwa mkuu wa FBI James Comey
Wabunge waandamizi nchini Marekani wamemtaka rais Donald Trump kusalimisha mazungumzo yoyote yaliorekodiwa kati yake na aliyekuwa mkurugenzi wa shirika la FBI James Comey aliyemfuta kazi.
Kiongozi wa Democrats katika bunge la seneti Charles Schumer alionya kuwa uharibifu wa kanda hizo utakuwa uvunjaji wa sheria.
Naye Seneta wa Republican Lindset Graham alisema kuwa Ikulu ya Whitehouse inahitaji kuwa wazi kuhusu iwapo kulikuwa na kanda zozote za rekodi za mazungumzo hayo au la.
Matamshi hayo yanajiri baada ya bwana Trump kusema katika mtandao wake wa Twitter matamshi yanayoonekana kuwa vitisho kwa mkuu huyo wa zamani wa FBI.
Alimuonya Comey wiki iliopita dhidi ya kuzungumza na vyombo vya habari akisema natumai hakuna rekodi za mazungumzo yetu.
Ikulu ya Whitehouse haijathibitisha wala kukana kuwepo kwa kanda hizo.
Bwana Schumer pia alionya kwamba masenata wa chama cha Democrats watakataa kumuunga mkurugenzi mpya wa FBI hadi pale mtaalam atakapochaguliwa kuchunguza hatua ya Urusi kuingilia maswala ya Marekani katika uchaguzi uliopita.
FBI inachunguza madai hayo pamoja na ushirikiano wa Urusi na kampeni ya rais Trump.
Rais Trump amekana uhusiano wowote na anasema bwana Comey amemhakikishia kwamba hachunguzwi.
Anasema kuwa alimpiga kalamu bwana Comey kwa sababu alikuwa ameshindwa kufanya kazi vizuri.
Wanachama wa Democrats wameshutumu Trump kwa kumfuta kazi Comey ili kujaribu kusitisha uchunguzi wa FBI.

source:bbc

Related Posts:

  • HALI TETE:Chenge agoma kuzungumza Vigogo waliotajwa katika ripoti ya pili ya kuchunguza makontena yenye mchanga wa madini (makinikia)  kuisababishia Serikali hasara ya matrilioni ya fedha kupitia sekta ya madini, walipokuwa wakihudumu katika nyadhifa … Read More
  • Hili ndilo janga la tatu alilolipata Mbowe Masaibu yanazidi kumkumba Mbunge wa Hai na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe baada ya Serikali kung’oa miundombinu ya umwagiliaji katika shamba lake.Hilo ni janga jingine kwa Mbowe baada ya miezi michache iliyopita kutaj… Read More
  • HIKI HAPA: alichokisema John Bocco Bocco (kulia) akikabidhiwa jezi ya Simba na rais wa klabu hiyo Evans Aveva, imeteka vichwa vya habari vya mitandao mbalimbali ambapo mashabiki wa Simba wameonyesha kufurahishwa na usajili huyo. UONGOZI wa Simba, jana umeta… Read More
  • Mzee Akilimali ataka kumpiku Manji, atangaza kuwania uenyekiti Yanga AKILIMALI Katibu Mkuu wa Baraza la Wazee wa Yanga, Ibrahimu Akilimali ametangaza kuwania nafasi ya uenyekiti wa klabu ya hiyo iliyoachwa wazi hivi karibuni na aliyekuwa mwenyekiti wa klabu hiyo, Yusuf Manji.Hivi karibuni M… Read More
  • AJALI:Gari la polisi laua bodaboda Gari la Polisi MTU mmoja amefariki dunia na mwingine kujeruhiwa baada ya pikipiki maarufu kwa jina la bodaboda waliyokuwa wakitumia kusafiri, kugongana uso kwa uso na gari la Jeshi la Polisi katika wilaya ya Rorya… Read More

0 comments:

Post a Comment