Watu wengi wanaotaka kununua simu janja/Sikanu (Smartphone), mojawapo ya jambo wanaloangalia pindi wafanyapo uchaguzi wa simu ni ukubwa wa uhifadhi wa ndani (storage).
Sababu kubwa ya kufanya hivyo ni kupata wasaa wa kusanidi (Install) App nyingi zaidi kadri iwezekanavyo, lakini hilo ni tofauti sana kwa Rais wa Marekani Donald Trump.
Kwa mujibu wa ripoti mpya imeelezwa Simu binafsi ya Rais wa Donald Trump imesanidiwa (Installed) App moja tu.
Mwandishi wa habari za kisiasa na mhariri wa AXIOS Media, Mike Allen, anasema Rais Trump anatumia simu ya iPhone na kwamba simu yake imewekwa App ya Twitter tu.
Sababu ya kufanya hivyo na kumuwekea App hiyo ni kupunguza hatari ya uwezekano wa simu yake kudukuliwa. Aidha pia kumpunguzia muda wa matumizi ya simu na ili ajielekeze zaidi katika mambo ya kio�si zaidi.
Muda mwingi hutumia kuangalia TV ili kujua matukio yanayoendelea duniani.
Simu ya awali ambayo alizuiwa kuitumia baada ya kuwa Rais ilikuwa ni Samsung. Alibadili kutoka Android kwenda iOS mwezi Machi mwaka huu.
Mpaka anaapishwa kuwa Rais wa Marekani inaelezwa simu aliyokuwa anatumia ni Samsung Galaxy S3 ambayo ilitolewa mwaka 2012.
Rais aliyepita Baraka Obama alisema wakati wa kuingia madarakani kwamba anatumia BlackBerry na matumizi yake yalikuwa ni kutuma ujumbe, kupiga picha na kusikiliza Muziki.
Chanzo: Teknokona
Friday, 2 June 2017
Home »
» App Pekee Iliyopo Kwenye Simu Anayotumia Rais wa Marekini Donald Trump
App Pekee Iliyopo Kwenye Simu Anayotumia Rais wa Marekini Donald Trump
Related Posts:
Kijana Marekani afariki baada ya kunywa kafeini nyingi kwa haraka Davis Cripe alikunywa vitaji tatu vya kafeini chini ya masaa mawili Kijana aliyekuwa buheri wa afya amefariki baada ya kunywa vinywaji vyenye kiwango cha juu sana cha kafeini (dutu inayopatikana katika vinywaji kama vile ka… Read More
Kirusi cha WannaCry kilitoka Korea Kaskazini? Ujumbe huu wa mtaalamu wa Google uliibua uwezekano wa kuhusika kwa Korea Kaskazini Nani alihusika katika shambulio la kirusi cha mtandaoni ambacho kiliathiri kompyuta katika zaidi ya mataifa 150 duniani, zikiwemo Kenya na T… Read More
Sababu ya Chui kula windo lake akiwa juu ya mti? Chui akimuwinda Swara Wanyama wengi wakiwemo wanyama wakubwa watano wa Afrika, hurandaranda katika mbuga ya wanyama pori ya Sabi Sand nchini Afrika Kusini. Wakati mwingine wanyama hawa hupatikana maeneo wasiyotarajiwa, kam… Read More
Uwezekano wa mimea ya msituni kutumiwa kupanga uzazi Je huenda kemikali kutoka kwa mimea ya msituni ikawa dawa mpya ya kupanga uzazi Kemikali mbili zinazopatikana katika mimea ya mistuni zinauwezo wa kutengeneza dawa za mpango wa uzazi, ikiwa wanasayansi wangejua wapi wangepa… Read More
Kijana aliyeunda setilaiti ndogo zaidi Indi Rifath aliviambia vyombo vya habari kuwa kifaa hicho kitafanya safari ya saa nne. Kijana mmoja nchini India ameunda kile kinachotajwa kuwa setilaiti ndogo zaidi ambayo itawekwa kwenye mzingo wa dunia katika kituo cha shirik… Read More
0 comments:
Post a Comment