Wednesday, 31 May 2017

Jeshi la Polisi Tanzania, latoa onyo

Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania Simon Sirro
Image captionMkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania Simon Sirro
Jeshi la Polisi nchini Tanzania limetoa onyo kwa wale wote wanaojihusisha na vitendo vya uhalifu na kusababisha mauaji ya raia na polisi.
Akizungumza kwa mara ya kwanza, mbele ya vyombo vya habari, baada ya kuteuliwa katika nafasi hiyo, siku chache zilizopita, Mkuu wa Jeshi la polisi Simon Sirro amesema changamoto iliyopo kwa sasa ni tatizo la mkoa wa Pwani ambako raia wema wamekuwa wakiuawa.
Katika kukabiliana na hali hiyo amesema wanaendelea na operesheni mbalimbali kuhakikisha kwamba vitendo hivyo haviendelei na wanaojihusisha na mauaji wakikamatwa hatua kali zitachukuliwa dhidi yao.
''..Suala la Ikwiriri suala la Rufiji ni suala la muda mfupi...'' Alisema Sirro
Amesisitiza kuwa wahalifu ni kikundi cha watu wachache na kijue kuwa wao ni Watanzania, hivyo haoni sababu waendelee kuwafanyia wenzao ubaya.
Rais wa Tanzania John MagufuliHaki miliki ya pichaAFP
Image captionRais wa Tanzania John Magufuli
Katika hatua nyingine, Jeshi la Polisi Tanzania limetangaza kutoa takriban dola elfu 5, ama shilingi milioni 10, kwa yeyote atakayetoa taarifa zitakazofanikishwa kukamatwa kwa wahalifu wa mauaji ya wananchi na polisi mkoani Pwani.
Katika siku za hivi karibuni Tanzania imeshuhudia mauaji yanayofanywa na watu wasio julikana katika wilaya za Rufiji, Mkuranga na Kibiti mkoani Pwani, hali ambayo imeleta wasiwasi kwa raia.

source:bbc

Related Posts:

  • Jambazi wa kike auawa na polisi Nairobi Mwanamke anayedaiwa kuwa jambazi sugu, ambaye amekuwa akipakia mtandaoni picha zake akiwa amejipodoa na kujipamba, ameuawa na polisi jijini Nairobi. Kijana huyo ambaye ametambuliwa kama Claire Mwaniki aliuawa na polisi alf… Read More
  • Trump amuonya mkuu wa FBI aliyefutwa James Comey Rais wa Marekani Donald Trump amemtahadharisha mkuu wa shirika la uchunguzi wa jinai FBI aliyefutwa kazi James Comey dhidi ya kufichua habari kwa vyombo vya habari. Bw Trump ameandika kwenye Twitter kwamba Bw Comey heri "a… Read More
  • Mwanamke ajioa baada ya kukosa mchumba Q May Chen Anasema kwamba ameamua kuafikia ndoto yake kupitia kupiga picha za harusi. Alijichagulia marinda yote manne na vito alivyovaa Mwanamke mmoja ambaye anaugua saratani ya matiti amejioa mwenyewe baada ya kusubiri mc… Read More
  • Shambulizi la uhalifu wa mtandao laathiri mataifa 99 duniani Sambulizi la kihalifu mitandaoni lililotendeka kupitia utumizi wa vifaa vinavyoaminika kuibwa kutoka kitengo cha ujasusi nchini Marekani NSA limeathiri mashirika tofauti duniani. Kampuni ya kulinda uhalifu wa mitandao Avas… Read More
  • AJUCO THIRD YEAR WATUNISHIWA MISULI NA RMA Katika kile ambacho hakikutarajiwa na mashabiki wengi wa AJUCO third year lakini kimewezekana ni baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-1 dhidi ya timu ya chuo cha wauguzi Songea maarufu kama RMA. Mechi hiyo ilichezwa katika… Read More

2 comments:

  1. Thank you so much for your visit in my blog, i real appreciate your concern. I promise i will visit your blog.

    Thank you
    Sonsoge from Tanzania.

    ReplyDelete
  2. I visited your blog , but unfortunately i don't understand your language.

    ReplyDelete