Tuesday, 16 May 2017

Mwanahabari mfichuzi wa mihadarati auwawa Mexico

Javier Valdez ameripoti pakubwa dhidi ya magenge ya ulanguzi wa mihadarati Mexico
Mwaandishi habari aliyeshinda matuzo mengi kuhusiana na taarifa zake nyingi ya ufichuzi wa shughuli za makundi, yanayojihusisha na ulanguzi wa dawa za kulevya nchini Mexico, ameuwawa.
Javier Valdez, aliuwawa na watu wenye silaha ambao walimiminia gari lake risasi akiwa katika mji wa Culiacán- jimbo la Sinaloa, kaskazini mwa nchi hiyo.
Javier Valdez aliuwawa alipokuwa akiliendesha gari lake kwenda ofisini kuliko na mtandao wake wa habari alilolianzisha huko Rio Doce.
Pia aliifanyia kazi shirika la habari la AFP, na gazeti moja maarufu nchini Mexico- La Jornada.
Rais wa Mexico, Enrique Pena Nieto, ameamuru uchunguzi ufanywe kuhusiana na kile alichosema uhalifu wa kutisha.
AFP nayo inasema kuwa Bwana Valdez alikuwa ameonyesha utendaki wa hali ya juu ya upekuzi dhidi ya walanguzi wa mihadarati, licha ya kufahamu kuwa alikuwa anahatarisha maisha yake.
Waandishi wanne wameuwawa nchini Mexico, katika kipindi cha miezi miwili iliyopita.
SOURCE:BBC

Related Posts:

  • Watu watatu wafa na mmoja kanusurika Rufiji Rufiji. Watu watatu  wamefariki dunia kwa kuzama majini na mmoja kunusurika kifo baada ya mtumbwi waliokuwa wakivukia kuzama bwawani wilayani Rufiji mkoani Pwani.Akithibitisha kutokea kwa vifo hivyo, Ofisa Tarafa … Read More
  • Ikulu yatoa majibu haya kwa Acacia Dar es Salaam. Uamuzi wa Serikali kuhusu suala la usafirishaji wa mchanga wa madini, utategemea ripoti ya kamati ya pili iliyoundwa na Rais John Magufuli kuchunguza suala hilo.Hayo yamebainishwa jana na Mkurugenzi wa M… Read More
  • Mgeja akasirishwa na kauli ya Polepole Morogoro. Mwenyekiti wa Tanzania Mzalendo Foundation, Khamis Mgeja amemuonya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Hampyrey Polepole aache mara moja kugeuza matukio ya kuuawa Watanzania katika Wilaya ya Mkuranga mkoa wa Pwani… Read More
  • Askofu Gwajima: nitawavua mataulo wanaonichokoza Dar es Salaam. Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima amewatahadharisha wanaomchokoza akisema ni sawa na mtu anayeanzisha ugomvi huku akiwa amevaa taulo.Akihubiri leo, Gwajima amesema wakiendelea atawavu… Read More
  • Askofu Gwajima afunguka juu ya sakata la madini Dar es Salaam, Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima amesema ni muhimu madini yasichimbwe hadi itakapowekwa mashine za kuchenjua makinikia.                   &nbs… Read More

0 comments:

Post a Comment