Monday 5 June 2017

Islamic State yakiri kufanya shambulio Londona

Kikosi maalumu cha kupambana na ugaidi London

Polisi nchini Uingereza wamekuwa wakifanya msako kwenye makazi manne mjini London hadi usiku wa manane kama sehemu ya uchunguzi juu ya shambulio la Jumamosi ambapo watu saba waliuawa na wengine wapatao hamsini walijeruhiwa .

Wachunguzi wanajaribu kubaini ikiwa wanaume watatu walioendesha basi lao dogo na kuwagonga wapita njia kabla ya kuwachoma visu wengine wengi walipata msaada wowote.

Watu kumi na mmoja wanashikiliwa kufuatia uvamizi wa polisi mashariki mwa London.

Kundi la Islamic State limesema lilihusika na shambulio hilo.

Mwanamke mmoja raia wa Canada aliyeuawa katika shambulio la London ametajwa katika vyombo vya habari.

Taarifa ya familia yake imesema kuwa alikuwa akifanya kazi katika hifadhi ya wasio kuwa na makazi kabla ya kuhamia Ulaya kuishi na mchumba wake.

Watu 21 waliojeruhiwa katika shambulio hilo wako katika hali mahututi.

0 comments:

Post a Comment